Monday, December 31, 2012

Migogoro ya ndoa, malezi mabovu chanzo cha watoto wa mitaani


TATIZO la watoto wa mitaani limekithiri nchini  licha ya jitihada zinazochukuliwa na Serikali, mashirika na watu binafsi.
Naandika makala haya baada ya kufanya uchunguzi binafsi kwa Jiji la Dar es Salaam nikifuatilia watoto hao.

Siyo siri kwamba ukifika Dar es Salaam hasa maeneo ya Kariakoo nyakati za usiku, utashangaa kuona watoto wengi wakiwa wamelala kwenye viambaza vya majengo mbalimbali.