TATIZO la watoto wa mitaani limekithiri nchini licha ya jitihada zinazochukuliwa na Serikali, mashirika na watu binafsi.
Naandika makala haya baada ya kufanya uchunguzi binafsi kwa Jiji la Dar es Salaam nikifuatilia watoto hao.
Siyo
siri kwamba ukifika Dar es Salaam hasa maeneo ya Kariakoo nyakati za
usiku, utashangaa kuona watoto wengi wakiwa wamelala kwenye viambaza vya
majengo mbalimbali.