Monday, January 28, 2013

Je, watoto wetu wanajifunza? Utafiti wa uwezo wa watoto kusoma na kuhesabu Tanzania 2010


Matokeo Muhimu

Je, watoto wetu wanajifunza?
Utafiti wa uwezo wa watoto kusoma na kuhesabu
Tanzania 20101
Utangulizi
Kote nchini, maendeleo makubwa yamefikiwa kwenye elimu ya msingi ndani ya
muongo (miaka 10) uliopita. Uandikishaji umepanda maradufu kote elimu ya msingi
na sekondari, na mamilioni ya watoto wameweza kwenda shule. Tanzania iko mbele ya
muda wa kutekeleza na kuyafikia malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) yanayohusu
upatikanaji wa elimu na usawa wa kijinsia katika elimu. Madarasa maelfu yamejengwa na
maelfu ya walimu wameajiriwa. Bajeti ya elimu imeongezeka mara tatu zaidi kwa kipindi
hiki; Serikali sasa inatumia dola za kimarekani zaidi ya bilioni moja kila mwaka au karibu
Sh 1 kwa kila Sh 5 ya bajeti ya elimu.
Mafanikio haya siyo hatua rahisi; yalihitaji dhamira kubwa ya kisiasa na mgawo mkubwa
wa fedha za umma. Wazazi pia wamejitahidi kugharamia sehemu yao, maana hata
ile elimu ya bure kiuhalisia sio bure, maana kuna gharama za sare za shule, vitabu,
kalamu, masomo ya ziada, usafiri na mengineyo. Swali la msingi hapa ni – Je, jitihada
na uwekezaji huu mkubwa umezaa matunda gani? Je, watoto wetu wanauwezo
wa kusoma na kufanya mahesabu? Mantiki ya elimu ni kumsaidia kila mtoto kukuza
maarifa ili aweze kuishi maisha yenye ustawi ndani ya dunia – kwa kuanza kujua kusoma
na kufanya mahesabu stadi ambazo zinaweka msingi wa uwezo wa kudadisi, kufikiri,
kusikiliza, kuuliza maswali, kuchambua, kupambanua na kuwasiliana kwa kujiamini. Je,
shule zetu zinafanikiwa kwenye jukumu hili? Watoto wetu wanajifunza?
Juhudi ya Uwezo imeundwa kujibu swali hili muhimu, na ripoti hii inawasilisha matokeo
ya utafiti wake wa kwanza. Uwezo ni juhudi ya miaka minne inayofuatilia ubora wa
1 Muhutasari huu umeandaliwa na Uwezo Tanzania (www.uwezo.net).
Uwezo iko ndani TEN/MET (www.tenmet.org) na ni sehemu ya juhudi pana
ya Afrika Mashariki inayoratibiwa na Twaweza (www.twaweza.org)
2
ujifunzaji mashuleni kwa kupima uwezo wa watoto wenye umri kati ya miaka 5 na 16
kusoma na kufanya hesabu kwa wanafunzi. Juhudi hii nchini Tanzania iko ndani ya TEN/
MET (Mtandao wa Elimu Tanzania, www.tenmet.org); na ni sehemu ya juhudi pana ya
Afrika Mashariki ukizijumuisha pia nchi za Kenya na Uganda inayoratibiwa na Twaweza
(www.twaweza.org). Upimaji umezingatia mbinu bora iliyothibitika iliyoandaliwa na
Kituo cha ASER nchini India, na inatumia mbinu ya kisayansi kupata sampuli nasibu ya
kaya nchi nzima. Watafiti waliopatiwa mafunzo walizitembelea kaya na kupima stadi za
kusoma (Kiswahili na Kiingereza) na kufanya Hisabati kwa kila mtoto kwa kutumia jaribio
fupi la ngazi ya darasa la 2. Ngazi ya darasa la 2 imechaguliwa kwa sababu kwa mujibu
wa viwango vya kimataifa na Tanzania hadi kufikia mwisho wa mwaka wa pili wa elimu ya
msingi kila mtoto anapaswa kuwa tayari ana stadi za msingi za kujua kusoma na kufanya
hesabu.
Upimaji wa kwanza wa Uwezo nchini Tanzania ulifanyika Mei 2010, baada ya maandalizi
makubwa na upimaji wa majaribio. Ulihusisha wilaya 38 kati ya wilaya 133 za Tanzania.
Katika kila wilaya vijiji 30 vilichaguliwa kwa nasibu, na katika kila kijiji watoto wote wenye
umri kati ya miaka 5-16 katika kaya 20 walipimwa. Kwa ujumla, watoto 42,033 katika kaya
22,800 walipimwa uwezo wao katika stadi za msingi. Matokeo sita muhimu ya upimaji
huo yanawasilishwa hapa chini. Ripoti kuu inaweza kuchukuliwa hapa www.uwezo.net
Matokeo Muhimu
1. Mhitimu mmoja kati ya
wahitimu watano hawezi
kusoma Kiswahili cha ngazi ya
darasa la 2
Japo Kiswahili ni lugha inayozungumzwa
kwa upana zaidi nchini, idadi kubwa ya
watoto hawawezi kusoma Kiswahili bila
shida. Kwenye sampuli zetu, chini ya nusu
(42.2%) ya watoto waliofanyiwa uchunguzi
waliweza kusoma kwa hatua ya hadithi.
Wakati watoto wote katika darasa la
3 wanapaswa kuweza kusoma hadithi
ya ngazi ya darasa la 2, watoto chini ya
mmoja kati ya 3 (32.7%) ndio wanaweza.
Watoto wengi hawajifunzi kusoma hadithi rahisi hadi wafikie darasa la 5 au la 6.
Hata hivyo, hadi wanamaliza shule ya msingi, mtoto mmoja kati ya 5 hawezi kusoma
hadithi ya ngazi ya darasa la 2. Licha ya kumaliza miaka saba ya elimu ya msingi,
watoto hao wanaelekea kubaki mbumbumbu (hawajui kusoma na kuandika) maishani
mwao.
3
ASILIMIA YA WATOTO WANAOWEZA KUSOMA KISWAHILI NGAZI YA DARASA LA 2
Darasa Hajui kitu Herufi Neno Aya Hadithi Jumla
Awali 53.5 27.7 2.7 2.5 13.6 100
Darasa la 1 41.8 37.8 10.6 4.2 5.6 100
Darasa la 2 24.1 32.3 17.0 9.8 16.8 100
Darasa la 3 14.8 20.0 16.4 16.1 32.7 100
Darasa la 4 9.6 14.7 12.0 16.6 47.1 100
Darasa la 5 6.0 10.1 7.4 13.8 62.8 100
Darasa la 6 4.0 6.1 4.9 11.1 73.9 100
Darasa la 7 1.8 5.9 3.3 8.0 81.0 100
Jumla 18.6 19.2 9.6 10.5 42.2 100
2. Nusu ya wanafunzi hawawezi kusoma Kiingereza cha ngazi ya
darasa la 2
Kiingereza ni somo gumu zaidi
kwa wanafunzi. Ingawa wanafunzi
wote wa darasa la 3 wanapaswa
kuweza kusoma Kiingereza cha
ngazi ya darasa la pili, chini ya
mwanafunzi 1 kati ya 10 (7.7%)
ndio anaweza. Maendeleo kwenye
somo la Kiingereza ni ya taratibu
sana; kwa darasa la tano, ni mtoto
1 tu kati ya watoto 4 anaweza
kusoma hadithi. Karibu nusu ya
wanafunzi hawawezi kusoma hata
maneno mafupi ya Kiingereza.
Watoto wengi wanafika darasa
la 7 bila kuwa na stadi zozote za
Kiingereza. Hadi wanamaliza shule
ya msingi, nusu ya wanafunzi (49.1%) bado hawawezi kusoma hadithi ya kiwango
cha darasa la 2 ya Kiingereza, na bila shaka wanafunzi wachache sana wanauwezo wa
kusoma kwenye ngazi ya darasa la 7. Hii ina maana kuwa idadi kubwa ya wanafunzi
wanaoingia sekondari hawawezi kusoma kwa lugha ya Kiingereza, ambayo ni lugha
ya kufundishia elimu ya sekondari.
4
ASILIMIA YA WATOTO WANAOWEZA KUSOMA KIINGEREZA NGAZI YA DARASA LA 2
Darasa Hajui kitu Herufi Neno Aya Hadithi Jumla
Awali 68.3 16.9 2.3 3.4 9.1 100
Darasa la 1 68.0 24.8 3.8 1.3 2.1 100
Darasa la 2 55.5 29.4 7.5 3.8 3.9 100
Darasa la 3 42.0 26.7 14.2 9.4 7.7 100
Darasa la 4 29.0 24.0 16.0 15.5 15.4 100
Darasa la 5 21.4 19.6 13.7 20.9 24.5 100
Darasa la 6 15.1 13.6 13.6 21.9 35.8 100
Darasa la 7 7.9 11.5 10.7 19.1 50.9 100
Jumla 37.8 21.0 10.4 12.1 18.7 100
3. Wahitimu 7 tu kati ya 10 wanaweza kufanya hesabu za ngazi ya
darasa la 2
Ingawa stadi za kuzidisha ziko kwenye
mtaala wa darasa la 2, wanafunzi
wachache tu wa darasa la 2 waliweza
kuzidisha bila shida. Zaidi ya
nusu ya wanafunzi hawawezi hata
kujumlisha. Hadi kipindi wanafika
darasa la 5, watoto wengi wanaweza
kutoa na kujumlisha, lakini wengi
bado hawawezi kuzidisha. Watoto
wengi wanapata stadi za Hisabati
mwishoni mwa shule ya msingi.
Hata hivyo, watoto 3 kati 10 (31.5%)
wa darasa la 7 bado hawawezi kufanya
hesabu za kuzidisha za ngazi
ya darasa la 2. Na mtoto 1 kati ya 10 anamaliza shule ya msingi bila kuwa na stadi
za Hisabati kabisa; hawezi hata kujumlisha hesabu ndogo. Hii inaweza kumaanisha
kuwa watoto wengi wanaojiunga na shule za sekondari hawana msingi imara kwenye
Hisabati ambao ni muhimu kwenye ujifunzaji na uchambuzi, hasa katika masomo ya
sayansi na biashara.
5
Kijijini
Mjini
Awali
Darasa I
Darasa II
Darasa III
Darasa IV
Darasa V
Darasa VI
Darasa VII
ASILIMIA YA WATOTO WANAOWEZA KUFANYA HISABATI NGAZI YA DARASA LA 2
Darasa Hajui kitu Namba Kujumlisha1 Kujumlisha2 Kutoa1 Kutoa2 Kuzidisha Jumla
Awali 40.0 41.9 2.7 1.6 1.7 1 11.0 100
Darasa la 1 26.5 56.9 9.2 1.9 2.3 1 2.4 100
Darasa la 2 15.7 45.8 16.9 4.9 5.5 4 7.6 100
Darasa la 3 9.9 30.3 20.0 8.5 7.3 6 18.5 100
Darasa la 4 7.2 22.0 14.1 10.0 7.0 7 32.8 100
Darasa la 5 5.1 13.9 11.0 10.3 6.7 7 45.8 100
Darasa la 6 3.3 9.2 7.7 10.2 5.9 6 57.8 100
Darasa la 7 2.2 7.9 4.8 7.0 4.7 5 68.5 100
Jumla 13.1 28.3 11.1 7.0 5.2 5 30.8 100
4. Watoto wa mijini hufanya vizuri zaidi kuliko wa vijijini
Watoto wa mijini hupata asilimia kati ya 7 na 10 zaidi kuliko watoto wa vijijini katika
masomo yote. Tofauti ni kubwa zaidi hususani katika madarasa ya 2-4, wakati watoto
wa mijini huanza kupata stadi za msingi ilhali wenzao wa vijijini wanaachwa nyuma.
Inaelekea kuwa watoto wa vijijini hatimaye huanza kupata stadi hizo za darasa la pili
wafikapo madarasa ya 6 na 7; lakini kuna uwezo mkubwa kuwa wanazidi kuporomoka
zaidi kwenye stadi ya kusoma katika ngazi yao
5. Wasichana hufanya vizuri kuliko wavulana
Wasichana walifanya vizuri zaidi katika masomo yote waliyopimwa, ingawa tofauti
ni ndogo sana. Kati ya watoto wote waliopimwa, 43.5% ya wasichana waliweza
kusoma hadithi katika Kiswahili ikilinganishwa na 40.7% ya wavulana. Katika masomo
ya Kiingereza na Hisabati tofauti ilikuwa ni ndogo mno, kama inavyooneshwa katika
jedwali hapo chini. Hata hivyo matokeo haya yanapingana na ile dhana ya muda mrefu
6
% Watoto
Hadithi ya Kiswahili Hadithi ya Kiingereza Kuzidisha
Wavulana
Wasichana
Hawako shule Awali Elimu ya watu wazima Msingi 1-4 Msingi 5-7 Sekondari +
% Watoto wanoweza kusoma
kuwa wasichana hawafanyi vizuri kama wavulana, na inaibua maswali kuhusu kwa nini
kunakuwa na tofauti kubwa katika matokeo ya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi
ambapo wavulana hung’ara zaidi. Hata hivyo, tofauti hizi ndogo zisifiche ule ukweli
mkubwa zaidi kuwa watoto wengi mno wasichana na wavulana hawana uwezo wa
kimsingi katika masomo ya lugha zote mbili na Hisabati.
6. Watoto wenye mama waliosoma hufanya vizuri zaidi
Watoto ambao mama zao wamesoma hadi elimu ya sekondari hufanya vizuri sana
kuliko watoto wengine. Kwa mfano, katika darasa la 3 na 4 watoto hawa wana
uwezekano wa mara tano zaidi kuweza kusoma hadithi ya Kiingereza na wana
uwezekano wa mara mbili zaidi kufanya Hisabati na kusoma hadithi ya Kiswahili. Hata
watoto ambao mama zao wamemaliza elimu ya msingi tu wanafanya vizuri kiasi kuliko
wale ambao mama zao hawajasoma kabisa. Tofauti katika matokeo huanza kujionesha
kuanzia darasa la kwanza hadi darasa la saba; ikiashiria kwamba elimu ya mama ni
muhimu katika ngazi zote za shule.
7
Hitimisho
Matokeo ya tathmini ya Uwezo iliyohusisha kaya zaidi ya 20,000 na watoto zaidi
ya 40,000 yanaonesha kuwa kuna tatizo kubwa katika elimu nchini Tanzania. Hadi
wanapoingia darasa la 3, watoto asilimia 100% wanapaswa kuwa na stadi za kusoma
na kuhesabu. Lakini ukweli ni kuwa hadi darasa la 3, watoto 7 kati ya 10 hawawezi
kusoma Kiswahili cha msingi; watoto 9 kati ya 10 hawawezi kusoma Kiingereza cha
msingi, na watoto 8 kati ya 10 hawawezi kufanya Hisabati za msingi.
Hata wanapofikia hatua ya kumaliza elimu ya msingi idadi kubwa mno ya watoto huwa
hawawezi kufanya kile ambacho walipaswa kuwa wana kijua miaka mitano iliyotangulia
wakati wakiwa katika darasa la 2. Mgawanyo kiwilaya unaonesha tofauti kubwa kati yao,
na ambapo baadhi ya wilaya ziko chini sana ya wastani wa kitaifa.
Ukweli ulio bayana ni kuwa, licha ya maendeleo makubwa yaliyofikiwa katika elimu
yaliyowezekana kutokana na kuwekezwa kwa matrillioni ya shilingi kila mwaka, idadi
kubwa sana ya watoto nchini Tanzania hawajifunzi.
Je, nini kifanyike kuhusu hali hii?
Kwanza, tunahitaji kutulia na kutafakari matokeo haya na kuchunguza yanamaanisha nini.
Kukimbilia kuyapuuza au kutunga masuluhisho ya haraka haraka pengine haitasaidia,
kwani inaweza kusababisha kushindwa kutambua kiini cha tatizo na hivyo kuchukua
hatua zisizofaa. Kushangilia majengo mapya na idadi kubwa ya watoto wanaoandikishwa
shule inaweza kuwa hatari kama matokeo yake ni kufunika ukweli kwamba idadi kubwa
ya watoto wanamaliza elimu ya msingi bila kujua kusoma na kuhesabu.
Pili, ingawa changamoto lazima ziwepo pale ambapo mfumo wa elimu unapopanuliwa
ghafla, bado tunaweza kuuliza: Je, mikakati ya kisera na malengo ya kisiasa yanalenga
mambo sahihi? Hivi sasa, nchini Tanzania na kwingineko, mkazo zaidi umewekwa
katika kupatikana kwa vitendeakazi kama vile madarasa, maabara, vitabu na walimu,
badala ya matokeo ya ujifunzaji. Mathalani, stadi za kusoma, kuhesabu, kuandika
udadisi na ubunifu. Kwa vile ushahidi unaonesha kuwa vitendeakazi havijaleta stadi hizi,
kuna umuhimu wa kupanga mfumo mzima wa elimu kulenga zaidi uwezo na stadi za
mwanafunzi, kuanzia ndani ya wizara zinazohusika na elimu, taasisi za elimu, watunga
mitaala, mitihani, tathmini ya walimu na shule, vipimo vya maendeleo na vipaumbele
vya kisiasa.
Tatu, kuna haja ya kuangalia zaidi nini kinachotokea shuleni kuliko kutazama takwimu
za kitaifa pekee. Tafiti zilizofanyika katika nchi nyingi zinaonesha kuwa mchakato wa
kufundisha na kujifunza unaweza kuwa na hitilafu kubwa. Mawili kati ya matatizo
ambayo hujitokeza mara kwa mara ni kuwa shule hazipati fedha za kutosha (yaani bajeti
za elimu zinazoongezeka zinatumika kwa mambo mengine badala ya kuboresha shule) na
kwamba walimu hawana motisha ya kutosha na hawafundishi (yaani muda wanaotumia
kufundisha darasani ni mdogo mno). Pengine itasaidia kuchambua mambo hayo mawili
8
kwa kina, na kutafuta namna ya kuyaboresha. Pia kuna haja ya kuangalia kwa makini
uhusiano kati ya rasilimali za kutosha kufika shuleni na walimu kuwapo kazini kwa
upande mmoja, na uwezo na stadi za mwanafunzi anapohitimu kwa upande mwingine.
Nne, uwazi zaidi unaweza kuwawezesha watunga sera na watu wengine kutafakari
na kuchukua hatua. Uwezo imedhamiria kusambaza matokeo ya tafiti zake ili kusaidia
kulifikia lengo hili. Lakini Serikali inaweza kwenda mbele zaidi ili kuwezesha data za kila
shule kupatikana kwenye mtandao, na katika vyombo vya habari kila afisa wa serikali
ya mtaa, mwalimu, mzazi na mwanafunzi alinganishe hali na utendaji wake na wa
wengine. Maendeleo ya teknolojia hasa usambazaji wa simu za mkononi vimewezesha
ubadilishanaji habari katika kiwango kikubwa na kufungua fursa mpya nyingi.
Tano, badala ya kuendelea kufanya kile ambacho kimeshafanyika kwa jitihada zaidi,
pengine umefika wakati wa kufanya kitu tofauti. Utafiti wa Uwezo na tafiti zilizofanyika
duniani zinaashiria kuwa kiini cha kitendawili hiki ni kuangalia upya suala la motisha ili
wadau muhimu katika sekta hii watambuliwe kwa kuhamasisha kujifunza. Wazo moja
ambalo linafaa kufikiriwa, na ambalo Rais Jakaya Kikwete kesha lipokea, linaitwa cash on
delivery au malipo baada ya matokeo (www.cgdev.org/section/initiatives/active/codaid).
Msingi wake mkuu ni kuwa kupatikana kwa fedha zaidi kwa kazi ya elimu kutategemea
kufikiwa kwa malengo (yaliyokaguliwa na shirika huru), kama vile kusoma na kuhesabu
(kwa mfano kwa kila mtoto anayemaliza elimu ya msingi akiwa na stadi zilizokubalika,
zitatolewa Sh laki tatu). Wazo hili linaweza kupanuliwa ili hizo Sh laki tatu zigawiwe kwa
viongozi wa eneo ilipo shule, walimu, na pengine hata wazazi. Lengo ni kuwashawishi
wadau wahusika kuzingatia na kutambua mafanikio katika kujifunza. Hakuna hakikisho
kuwa wazo hili litafanikiwa. Lakini katika hali ya kuwepo kwa tatizo kubwa linaloikabili
sekta ya elimu Tanzania kwa sasa, hasa pale ambapo njia za kawaida zimeshindwa kuleta
mafanikio ya maana, kufanya majaribio mbadala yaliyofikiriwa kwa makini kama hii
ya malipo baada ya matokeo, na kisha kuchunguza matokeo yake inaweza kutusaidia
kusonga mbele.
Matokeo ya utafiti wa Uwezo yanazinduliwa katika kipindi cha kuelekea Uchaguzi Mkuu
nchini Tanzania. Vyovyote matokeo ya siasa yatakavyokuwa, miaka mitano ijayo inatoa
fursa ya kulitazama sakata la elimu kwa uwazi, ujasiri na kwa njia itakayoleta mafanikio.
Ni watu wenye stadi, uwezo na wanaojiamini watakao liwezesha taifa letu kuneemeka
hususani katika muktadha wa ushirikiano wa Afrika Mashariki na katika hali ya
utandawazi. Yeyote atayechaguliwa kuwa Rais ajaye wa Tanzania, kazi ya kuibadili elimu
kutoka kuangalia vitendeakazi hadi kuhakikisha kila mtoto anaweza kusoma na kuhesabu
na kujifunza pengine ndicho kitakuwa kipimo kikuu cha mafanikio ya uongozi wake.

No comments:

Post a Comment